KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

October 8, 2016

MKEMIA MKUU AWAPA ZAWADI WANAFUNZI BORA SAYANSI

02
Mkemia Mkuu wa Serikali, Profesa Samwel Manyele (kulia), akitoa hotuba wakati wa hafla ya utoaji zawadi kwa wanafunzi na walimu Bora wa masomo ya Kemia na Baiolojia kwa kidato cha Nne na kidato Tano 2014/2015 iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali.
01
Mgeni Rasmi, Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Bw. Michael John (kulia) akitoa hotuba kabla ya kukabidhi zawadi kwa Wanafunzi na Walimu Bora wa masomo ya Kemia kwa Kidato cha Nne waliomaliza mwaka 2014 na cha Sita 2015. Jumla ya wanafunzi Ishirini na Nne (24) na walimu wane (4) walifanikiwa kupewa zawadi kwenye hafla iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ofisi za Mkemia Mkuu wa Serikali, Jijini Dar es Salaam.
03
Mhariri Mtendaji wa Magazeti ya Serikali, Dkt. Jim Yonazi (kulia) akitoa neno la shukrani kwa niaba ya wazazi wa wanafunzi waliopata zawadi kwa kufanya vizuri kwenye masomo ya Kemia na Baiolojia kwa Kidato cha Nne 2014 na Kidato cha Tano 2015. Dkt Yonazi alimsindikiza kijana wake Yonazi Charles Senkondo kwenye hafla hiyo
6
 Mwanafunzi Bora wa masomo ya Kemia na Baiolojia kwa upande wa wasichana wa kidato cha sita mwaka 2015, Meghna Solanki (kulia) akitoa neno la shukrani kwa niaba ya wanafunzi wenzake baada ya kupatiwa zawadi zao
07
 Wanafunzi Bora wa masomo ya Kemia na Baiolojia kwa Kidato cha Nne na Tano kwa mwaka 2014/2015 wakitambulishwa wakati wa hafla ya kuwapa zawadi iliyofanyika kwenye viwanja vya Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Jijini Dar es Salaam.
08
Mgeni Rasmi, Bw. Michael John, akimkabidhi zawadi mwanafunzi, Yonazi Charles Senkondo (kulia) baada ya kuwa mwanafunzi bora kwenye masomo mawili ya Kemia na Baiolojia kwa kidato cha Sita mwaka 2015.

No comments:

Post a Comment