KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

October 9, 2016

SHEREHE ZA MWENGE WA UHURU ZILIVYOFANA WILAYANI KISHAPU

Habari na Picha na Robert Hokororo
Mwenge wa Uhuru umewasili na kupokelewa katika Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu ukitokea Manispaa ya Shinyanga mkoani Shinyanga.
Uliwasili majira ya saa 2 asubuhi katika Kijiji ya Bubiki ambapo Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Josephine Matiro alimkabidhi mwenzake wa Wilaya ya Kishapu, Nyabaganga Taraba kabla ya kuanza mbio zake kukagua na kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo.
Ukiwa wilayani humo ulizindua miradi 11 yenye thamani ya sh. bilioni 1.6 ikiwemo ule wa maji kutoka Ziwa Victoria mkoani mwanza unaotarajiwa kuanza kuwanufaisha wakazi wa Kishapu hivi karibuni.
Mara baada ya kuwasili wilayani humo mbio za Mwenge wa Uhuru zikiongozwa na Mkuu wa wilaya hiyo na viongozi mbalimbali ulianza mbio zake kuelekea katika mradi wa kwanza wa vyumba vipya vya madarasa na matundu ya vyoo.

 Mwenge wa Uhuru ukikimbizwa katika maeneo mbalimbali mara baada ya kuwasili wilayani Kishapu.
 Viongozi mbalimbali wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Kishapu, Nyabaganga Taraba wakisubiri kukabidhiwa Mwenge wa Uhuru wilayani humo katika Kijiji cha Bubiki.
 Kikundi cha ngoma cha Makirikiri kikionresha manjonjo yake katika ufunguzi wa mradi wa stendi kuu ya mabasi na kituo cha polisi eneo la Mhunze wilayani Kishapu wakati wa mbio za Mwenge wa Uhuru.

No comments:

Post a Comment