KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

October 3, 2016

TANESCO DODOMA YAOMBA KUPEWA HADHI YA MKOA MAALUM

index*Ni katika kukabiliana na ujio wa Serikali Dodoma
MENEJA wa Shirika la Ugavi wa Umeme Tanzania (TANESCO) mkoa wa Dodoma, Mhandisi Zakayo Temu amesema ni vema mkoa huo ukapewa hadhi ya mkoa maalum ili uweze kukabiliana na changamoto za ujio wa Serikali Dodoma.
Ametoa ombi hilo jana jioni (Jumapili, Oktoba 2, 2016) wakati akitoa taarifa ya utendaji wa TANESCO Mkoa wa Dodoma mbele ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ambaye alifika kwenye kituo cha kupozea umeme cha Zuzu nje kidogo ya mji wa Dodoma, kukagua mahitaji halisi ya umeme ikilinganishwa na ujio wa watumishi mkoani humo.
Mhandisi Temu alisema: “Tunaomba mkoa wetu wa Dodoma ambao ni Makao Makuu uangaliwe kwa jicho la pekee na kupewa hadhi ya mkoa maalum kama ilivyo kwa Dar es Salaam ambako kuna mikoa minne ya ki-TANESCO.”

No comments:

Post a Comment