KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

October 28, 2016

TANZANIA YAWAKARIBISHA WAKOREA KUSINI KUWEKEZA SEKTA YA VIWANDA

sou1
Mkurugenzi wa Uhamasishaji uwekezaji kutoka Kituo cha Uwekezaji Tanzania-TIC, John Mnali (Katikati), akibadilishana mawasiliano na mmoja wa wafanyabiashara walioonesha nia ya kuweka nchini Tanzania baada ya Mkurugenzi huyo kuwasilisha mada kuhusu fursa za uwekezaji zinazopatikana Tanzania, wakati wa mkutano wa 5 wa ushirikiano wa kiuchumi kati ya Korea ya Kusini na nchi za Afrika (KOAFEC), Jijini Seoul, Korea Kusini.
sou2
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango (Mb), akibadilishana mawasiliano na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya MarineBio, Heo Yun-Young, ambaye kampuni yake inataka kuwekeza kiwanda cha kusindika zao la mwani linalopatikana katika Bahari Kuu ya Hindi nchini Tanzania
sou3
Msaidizi wa Waziri wa Fedha na Mipango, Edwin Makamba, akiwa katika picha ya pamoja na Mwenyekiti ambaye pia ni Rais wa Benki ya EXIM ya Korea Kusini, Lee Duk-Hoon baada ya hafla ya usiku ya kuagana kwa washiriki wa mkutano wa Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Korea Kusini na Nchi za Kiafrika, Jijini Seoul, nchini Korea kusini.
sou4
Mkurugenzi wa Uhamasishaji uwekezaji kutoka Kituo cha Uwekezaji Tanzania-TIC, John Mnali, akiwasilisha mada kuhusu fursa za uwekezaji zinazopatikana Tanzania, wakati wa mkutano wa 5 wa ushirikiano wa kiuchumi kati ya Korea ya Kusini na nchi za Afrika (KOAFEC), Jijini Seoul, Korea Kusini
sou6
Maofisa kutoka wizara ya Fedha na Mipango, Edwin Makamba ambaye ni msaidizi wa Waziri wa Fedha na MIpango, kushoto, na Mkuu wa idara ya Sera, Shogolo Msangi, wakifuatilia uwasilishwaji wa mada kuhusu fursa za uwekezaji zilizopo Tanzania Bara na Tanzania Visiwani, wakati wakati wa mkutano wa 5 wa ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Korea Kusini na nchi za Kiafrika, uliomalizika leo Jijini Seoul, Korea Kusini
sou7
Mkuu wa kitengo cha utafutaji Rasilimali, kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Zanzibar, Sabra Issa Machano, akiwasilisha mada kuhusu fursa za uwekezaji zinazopatikana Tanzania Zanzibar, wakati wa mkutano wa 5 wa ushirikiano wa kiuchumi kati ya Korea ya Kusini na nchi za Afrika (KOAFEC), Jijini Seoul, Korea Kusini.
sou8
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), akimpongeza Mkuu wa kitengo cha utafutaji Rasilimali, kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Zanzibar, Sabra Issa Machano, baada ya akiwasilisha mada kuhusu fursa za uwekezaji zinazopatikana Tanzania Zanzibar, wakati wa mkutano wa 5 wa ushirikiano wa kiuchumi kati ya Korea ya Kusini na nchi za Afrika (KOAFEC), Jijini Seoul, Korea Kusini.

No comments:

Post a Comment