KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

October 2, 2016

WAFANYAKAZI TBL WASHIRIKI KUPANDA MITI

Katika kutekeleza mkakati wa kampuni wa kutunza mazingira na sera ya wafanyakazi kutumia muda wao kwa ajili ya kazi za kijamii,wafanyakazi wa TBL Group wameungana na viongozi wa serikali na wafanyakazi wa taasisi mbalimbali za kiserikali na za binafsi katika kampeni ya uhamasishaji upandaji miti inayojulikana kama Mti Wangu.
Kampeni hii imezinduliwa leo na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mh.Samia Suluhu Hassan katika eneo la viwanja vya Gymkhana.
mti-wangu-3Diwani wa kata ya Kivukoni manispaa ya Ilala Henry Massaba wa pili (kushoto)  akimkabdhi mti wa kupanda  Meneja Ufanisi wa Uzalishaji Charles Nkondola Charles Nkondola  kwa niaba waya wafanyakazi wa TBL Group wakati wa uzinduzi wa  kampeni ya ‘Mti Wangu’ .Kushoto ni Meneja wa Afya na USalama, Renatus Nyanda.
mti-wangu-10Wafanyakazi wa TBL wakishiriki katika zoezi la kupanda miti katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam.
mti-wangu-11Wafanyakazi wa TBL wakishiriki katika zoezi la kupanda miti katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment