KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

April 27, 2017

BASHE 'AICHANA KENYA' KWA KUZUIA GESI YA TZ

Mbunge wa Nzega mjini, Hussein Mohamed Bashe amesikitishwa na Serikali ya Kenya kuweka zuio la kuingiza mitungi ya gesi inayotoka Tanzania kwa kusema ni vizuri nchi hiyo ikaheshimu mikataba ya 'East African Community (EAC)' .

Bashe amesema hayo baada ya serikali ya Kenya kupitia Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Andrew Kamau kupiga marufuku uagizaji wa gesi ya kupikia kutoka Tanzania kupitia mipaka ya nchi hiyo.

"Serikali ya Kenya imezuia gesi za matumizi ya nyumbani zinazotoka Tanzania kuingia Kenya ni vizuri Kenya ikaheshimu 'EAC treaty common'......Dar es salaam 'port and Cost' ya gesi inayotoka Tanzania ndiyo 'competetive edge' ya makampuni ya Tanzania dhidi ya yale ya Kenya uamuzi huu si sawa". Ameandika Bashe kupitia ukurasa wake wa twitter.

No comments:

Post a Comment