KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

May 21, 2017

KOREA KASKAZINI YARUSHA KOMBORA JINGINE

Korea Kaskazini yalifanyia majaribio kombora lingine
Korea Kaskazini yalifanyia majaribio kombora lingine 
Jeshi la Korea Kusini linasema kuwa Korea Kaskazini imefanyia majaribio kombora lingine.
Ofisi ya kijeshi nchini Korea Kusini inasema kuwa kombora hilo lilirushwa siku ya Jumapili jioni saa za Korea.
Jaribio hilo linafanyika wiki moja baada ya Korea Kaskazini kulifanyia majaribio kombora lingine ambalo inadai kuwa ni jipya na ambalo lina uwezo wa kubeba silaha kubwa ya nuklia.
Jumatatu iliyopita baraza la usalama la Umoja wa Mataifa liliitaka Korea Kaskazinia kusitisha majaribio kama hayo.
Ulisisitiza umuhimu wa nchi hiyo kuachana na hatua hizo.
Korea Kaskania inafahamika kwa kuunda zana za nuklia na imefanya jumla ya jaribio matano ya nuklia na ya makombora yenye uwezo wa kosafirisha zana hizo hadi maeneo inayolenga.
Korea Kusini inasema kuwa jaribio la hivi punde lilifanyiwa eneo la Pukchang magharibi mwa nchi.

No comments:

Post a Comment