Rais wa Shirikisho la Mpira wa
Miguu Tanzania, Jamal Malinzi amempongeza Mjumbe wa Kamati ya Utendaji
wa TFF, Ahmed Mgoyi kwa utumushi mara baada ya kutangaza kutowania
nafasi yoyote ya uongozi.
Mjumbe Mgoyi anayewakilisha Mikoa
ya Kigoma na Tabora aliandika waraka jana Juni 15, 2017 akielezea
kutogombea tena katika Uchaguzi wa TFF unaotarajiwa kufanyika Agosti 12,
mwaka huu.
“Nimefanya kazi na Wajumbe wangu
wote wa Kamati ya Utendaji. Tumefanya kazi kwa uadilifu mkubwa. Wakati
Tukielekea kwenye uchaguzi, mwenzetu ametangaza kutogombea tena, lakini
kwa namna nilivyofanya naye kazi, kwangu mimi naamini anahitajika mno,
lakini uamuzi wake ni mwisho unakuwa ni wa kwao.
“Naamini kwamba bado ni
mwanafamilia wa mpira wa miguu na pindi atakapohitajika kwa lolote lile
kama vile ushauri na masuala mengine, basi hatutasita kuwafuata kwa
sababu lengo ni kujenga na kuendeleza mpira wetu,” amesema Malinzi.
Katika ujumbe wake, Rais Malinzi
amesema kwamba hadhani kama Mgoyi hao atasita au kukataa kutoa
ushirikiano kwa uongozi wa shirikisho pindi akihitajika kutoa msaada wao
wa mawazo na ushauri.
Rais Malinzi amemtakia kila la
kheri katika majukumu yake mengine aliyojipangia kuyafanya huku akiwa
bado mwanafamilia wa mpira wa miguu
No comments:
Post a Comment